Thursday, July 4, 2013

Recipe For The HEART (Chakula Kifaacho kwa MOYO).



Habari za Mchana rafiki zangu

Napenda kuwakaribisha kwenye blog hii,hapa tunajadili aina za vyakula ambavyo hutumika kama tiba mbadala kwa magonjwa ambayo tunakumbana nayo katika maisha ya kila siku.
Mfululizo wa mwangaza huu ambao nimeona nitumie na rafiki zangu utakuwa kama mwanzo wa maisha mapya maana kwa kiwango kikubwa tafiti zimeonyesha ni kwa jinsi gani mlo mzuri na uliokamilika (balanced Diet) huchangia kwa asilimia sitini(60%) katika kurefusha maisha hasa kwa kikazi hiki tulichonacho.


                                                                Aubergine (Artichoke)

Leo nitapenda  kuongelea chakula au vyakula ambavyo hushauriwa kutumiwa mahususi kwa kujenga kiungo muhimu kwa binadamu kijulikanacho kama Moyo.

Moyo ni kiungo katika mwili ambacho huduma yake kwetu ni kubwa na hivyo huitaji uangalizi wenye mapenzi ya dhati na kuujali kwa kiwango cha hali ya juu,leo nimeanda aina mbili ya vyakula na kinywaji ambacho hupaswa kusaidia kuboresha na kujenga Moyo bila kusahau kuuepusha na magonjwa kama Presha n.k

Mchemsho wa Mbogamboga (Mixed Vegetables)

MAHITAJI
-250g  ya Njegere(peas) au Green Beans
-500g  ya Aubergine
-250g  ya Carrots
-100g  ya Maharage Soya
-400g  ya Viazi Mviringo
-01 Kitunguu
-02 Tangawizi

MAANDALIZI

-Hakikisha kimeoshwa vyema tayari kwa kupikwa
-Menya kama itakuwa ni njegere au maharage ya kijani vyema
-Kisha katakata Aubergine vipande vidogo vidogo kisha kwa ziada unaweza nyunyizia limao kuleta ladha
-Kisha chemsha kwa muda wa dakika thelathini(dk 30)


Mlo huu husaidia kuongeza madini na vitamini kwenye moyo.

Pia chakula hiki hushauriwa kwa watu wenye matatizo ya

Arterial Hypertension- kwa kuwa mchanganyiko huu wa mboga una kiwango kikubwa cha Potassiamu na pia Sodium katika kiwango cha chini hivyo kusaidia kuzuia Presha ya kupanda (High Blood Pressure) pia uhamasisha uzalishaji wa uchafu maji(diuresis- Urine Production)


Imeandaliwa
Dr Naomi J.K Mdongo

Presented by
Millan Abraham.
                                                              Bon Appertite


No comments:

Post a Comment